1
Ewe Roho wa mbinguni, maombi sikia! Makao yako yafanye, mioyoni mwetu.
2
Kama nuru tupenyeze, giza uondoe, Siri yako tuione, na amani yako.
3
Kama moto tusafishe, choma dhambi yetu, Roho zetu ziwe zote, hekalu la Bwana.
4
Kama umande na uje, utuburudishe, Moyo mkavu utakuwa, ni wenye baraka.
5
Kama upepo Ee Roho, katika pentekoste Ukombozi utangaze, kwa kila taifa.