1
U Mtakatifu! Mungu Mwenyezi! Alfajiri sifa zako tutaimba, U Mtakatifu, Bwana wa huruma, Mungu wa vyote, hata milele.
2
U Mtakatifu! Na malaika, Wengi sana wanakuabudu wote. Elfu na maelfu, wanakusujudu, Wa zamani na hata milele.
3
U Mtakatifu! Ingawa giza, Lakuficha fahari tusiione, U Mtakatifu! Wewe peke yako, Kamili kwa uwezo na pendo.