1
Twamsifu Mungu, Mwana wa upendo, Aliyetufia na kupaa juu.
Kiitikio
Aleluya! usifiwe, Aleluya! Amin; Aleluya! usifiwe, utubariki.
2
Twamsifu Mungu, Roho Mtukufu, Akatufunulia Mwokozi wetu.
3
Twamsifu Mwana, aliyetufia, Ametukomboa na kutuongoza.
4
Twamsifu Mungu, wa neema yote, Aliyetwaa dhambi akazifuta.
5
Tuamshe tena, tujaze na pendo, Moyoni uwashe moto wa Roho.