1
Nena rohoni Yesu, nena kwa upole, Sema kwangu kwa pendo, “huachwi upweke,” Fungua moyo wangu, nisikie mara, Jaza roho na sifa, sifa zako Bwana.
Kiitikio
Kila siku unene, vile kwa upole. Nong’oneza kwa pole, upole wa pendo, “Daima utashinda, uhuru ni wako.” Nisikie maneno, “huachwi upweke.”
2
Nena kwa wana wako, waonyeshe njia, Wajaze kwa furaha, fundisha kuomba, Wajifunze kutoa, maisha kamili, Wahimize ufalme, tumwone Mwokozi.
3
Nena kama zamani, ulipoitoa, Sheria takatifu, niishike pia, Nipate kutukuza Wewe Mungu wangu, Mapenzi yako tena, daima kusifu.