16

Bwana Ninakuhitaji

1

Bwana ninakuhitaji, Ni mpofu, maskini, Unishike mkononi, kwako napata nguvu.

Kiitikio

Kila saa, kila saa, Bwana ninakuhitaji, Kila saa, kila saa, unilinde kila saa.

2

Univike na mavazi, ya usikivu wako, Nguo zangu zote chafu, nazitamani zako.

3

Wewe ukiniongoza, nitakwenda salama, Nenda nami siku zote, u nuru na uzima.

4

Na ikiwa huko mbele, sehemu yangu ngumu, Au ikiwa furaha, unilinde kila saa.