1
Huniongoza Mwokozi, ndipo nami hufurahi, Niendapo pote napo, ataniongoza papo.
Kiitikio
Kuongoza hunishika, kwa mkono wa hakika, Nitaandamana naye, Kristo aniongozaye.
2
Pengine ni mashakani, nami pengine rahani, Ni radhi ijayo yote, yupo nami siku zote.
3
Mkono akinishika, kamwe sitanung’unika, Atakachoniletea, ni tayari kupokea.
4
Nikiisha kazi chini, sitakimbia mauti, Kushinda ni ya hakika, nikiongozwa na Baba.