200

Baba Yetu Aliye Mbinguni

1

Baba yetu aliye mbinguni, amenifurahisha yakini, Kuniambia mwake chuoni, ya kuwa nami Yesu pendoni.

Kiitikio

Anipenda Mwokozi Yesu, anipenda, anipenda, Anipenda Mwokozi Yesu, anipenda mimi.

2

Nimuachapo kutanga mbali, yeye yu vivyo hupenda kweli, Hunirejeza kwake moyoni, kweli yu nami Yesu pendoni.

3

Anipenda, nami ninampenda, kwa wokovu alionitenda, Akanifilia Msalabani, kwa kuwa nami Yesu pendoni.