1
Kuna mvua ya baraka, Bwana nimesikia, Unawamwagia wote, bure wanaipata.
Kiitikio
Na mimi, Na mimi, Bwana uninyeshee?
2
Sinipite Baba Mwema, dhambini nimezama, Rehema ni za daima, Bwana, unioneshe.
3
Sinipite, Yesu mwema, niwe nawe daima, Natamani kukwandama, Bwana, unichukue.
4
Sinipite, Roho Mwema, Mpaji wa uzima, Nawe shahidi wa wema, Bwana wema unipe.