44

Hakuna Rafiki Kama Yesu

1

Hakuna rafiki kama Yesu, hakuna, hakuna, Tabibu mwingine wa rohoni, hakuna, hakuna.

Kiitikio

Yesu ajua shida zetu, daima ataongoza, Hakuna rafiki kama Yesu, hakuna, hakuna,

2

Wakati ambapo hapo yeye, hapana, hapana, Wala giza kututenga naye, hapana, hapana.

3

Aliyesahauliwa naye, hakuna, hakuna, Mkosaji asiyempenda, hakuna, hakuna.

4

Kipawa kama Mwokozi wetu, hakuna, hakuna, Ambaye atanyimwa wokovu, hakuna hakuna.