56

Walio Kifoni

1

Walio kifoni nenda waponye, Uwatoe walio shimoni, Wanaoanguka uwainue, Habari njema uwajulishe.

Kiitikio

Walio kifoni, waokoeni, Mwokozi yuko huwangojea

2

Wajapokawia anangojea, Awasubiri waje tobani, Mwokozi hawezi kuwadharau, Huwasamehe tangu zamani.

3

Na ndani ya moyo wa mwanadamu, Huwamo shida tena huzuni, Lakini kwa Yesu kuna rehema, Kuwaponya na kuwaokoa.

4

Walio kifoni nenda waponye, Kazi ni yetu zawadi iko, Nguvu kuhubiri Bwana hutoa, Kwa subira tuwavute sasa.