1
Salama tumepita, safarini juma hii, Tumwendee Mwokozi, atubariki sasa, Siku hiyo ya raha, siku bora ya juma, Siku hiyo ya raha, siku bora ya juma.
2
Utupe nuru leo toka hazina yako, Ondoa dhambi zetu, tupokee na pendo, Mikono yapumzika, tuishi ndani yako, Mikono yapumzika, tuishi ndani yako.
3
Twakusanyika hapa, tusifu jina lako, Ukaribie kwetu, tupe neema Bwana, Utamu tusikize, wa raha ya milele, Utamu tusikize, wa raha ya milele.
4
Injili yako leo, ishike wenye dhambi, Itupe nguvu nyingi, iponye wenye shida, Mioyo yetu shangaza, vyakula utulishe, Mioyo yetu shangaza, vyakula utulishe.