103

Yesu Huita kwa Upole

1

Yesu huita kwa upole mwingi, atwita wewe nami, Moyoni mwetu hungoja hukesha, hukungojea wewe

Kiitikio

“Njoni, kwangu, mliochoka njoni” Yesu huita kwa upole mwingi, akwita, “uje kwangu”.

2

Atuombeapo usikawie, hutuombea sisi, Usidharau wema na huruma, huruma kwetu sisi.

3

Siku za maisha hupita hima, hupita kwako kwangu, Usiku waja kifo kinakuja, huja kwao na kwangu.

4

Fikiri juu ya upendo wake, upendo kwako kwangu; Dhambi zetu amekwisha samehe, msamaha ni wetu.