1
Sauti ni yake Bwana, “Kwenda nani tayari? Mavuno yanakawia, nani atayavuna? Kwa kudumu anaita, zawadi atatoa, Nani atakayejibu, “Nipo Bwana nitume.”
2
Kama huwezi safari, hata nchi za mbali, Pana watu karibuni, wasiomjua Yesu, Kama huwezi kusema, jinsi ya malaika, Waweza kuutangaza, upendo wa Mwokozi.
3
Ingawa huwezi kuwa, mkesha mlangoni, Ukiwatolea watu, nafasi ya uzima, Kwa sala na kwa sadaka, watoa msaada, Kama Haruni mwaminifu, kuinua mikono.
4
Roho za watu zikifa, Bwana akikuita, Usiseme kwa uvivu, “Hakuna kazi kwangu.” Kwa furaha anza kazi, ile aliyokupa, Ukajibu mara moja, “Nipo Bwana, nitume.”