1
Tabibu mkuu huyu, Yesu mwenye huruma, Atuletaye faraja, Yesu Mwokozi wetu.
Kiitikio
Imbeni malaika, sifa za Bwana wetu, Jina la pekee kwetu, ni la Yesu Bwana.
2
Mwana Kondoo msifuni, msifuni Mwokozi; Hatia zote na dhambi, huziondoa Yesu.
3
Hakuna jina jingine, linalofaa sifa, Au kutufurahisha, isipokuwa lake.
4
Naye atakapokuja, na utukufu wake, Tutafurahi milele, kukaa kwake Bwana.