1
Damu imebubujika, ni ya Imanweli, Wakioga wenye taka, husafiwa kweli.
2
Ilimpa kushukuru, mwivi mautini, Nami nisiye udhuru, yanisafi ndani.
3
Kondoo wa kuuawa, damu ina nguvu, Wako wote kuokoa, kwa utimilivu.
4
Bwana tangu damu yako, kunisafi kale, Nimeimba sifa zako, ‘taimba milele.
5
Bwana, umenikirimu, nisiyestahili Kwa damu yako sehemu, ya mali ya kweli.
6
Nikubali kukwimbia, mbinguni milele. Mungu nitamsifia, jina lako pekee.