115

Naendea Msalaba

1

Naendea msalaba, ni mnyonge mpofu, Yapitayo naacha, nipe msalaba tu.

Kiitikio

Nakutumaini tu, ewe Mwana wa Mungu; Nainamia kwako, niponye sasa Bwana.

2

Nakulilia sana, nalemewa na dhambi, Pole Yesu asema, “Nitazifuta zote.”

3

Natoa vyote kwako, nafasi nazo nguvu, Roho yangu na mwili, viwe vyako milele.

4

Kwa damu yake sasa, amenivuta sana, Upendo hubidisha, nimtafute Mwokozi.