118

Nilipotoka Kabisa

1

Nilipotoka kabisa, sasa narudi, Nikakawia dhambini, Bwana narudi.

Kiitikio

Narudi nyumbani, daima kwako, Kwa upendo nipokee, naja nyumbani.

2

Nikasusurika sana, sasa narudi, Mwenye uchungu natubu, Bwana narudi.

3

Nimechoka maovuni, sasa narudi, Pendo lako lanivuta, Bwana narudi.

4

Ndilo tumaini langu, sasa narudi, Yesu alinifilia, Bwana narudi.

5

Damu yake yanitosha, sasa narudi, Unioshe kenyekenye, Bwana narudi.