126

Nina Haja Nawe

1

Nina haja nawe, kila saa, Hawezi mwingine, kunifaa.

Kiitikio

Yesu nakuhitaji, vivyo kila saa, Niwezeshe Mwokozi, nakujia.

2

Nina haja nawe, kaa nami, Na maonjo haya, hayaumi.

3

Nina haja nawe, kila hali, Maisha ni bure, uli mbali.

4

Nina haja nawe, nifundishe, Na ahadi zako, zifikishe.

5

Nina haja nawe, mweza yote, Ni wako kabisa, siku zote.