1
Nionapo amani kama shwari, au nionapo shida, Kwa hali zote umenijulisha, ni salama rohoni mwangu.
Kiitikio
Salama rohoni, ni salama rohoni mwangu.
2
Ingawa Shetani atanitesa, nitajipa moyo kwani, Kristo ameona unyonge wangu, amekufa kwa roho yangu.
3
Dhambi zangu zote wala si nusu, huwekwa msalabani, Wala sichukui laana yake, ni salama rohoni mwangu.
4
Ee Bwana himiza siku ya kuja, panda itakapolia, Utakaposhuka sitaogopa, ni salama rohoni mwangu.