1
Saa heri ya sala, tunapojidhili, Kama tukija kwake Yesu rafiki, Tukiwa na imani, kwamba yu mlinzi, Waliochoka sana, watapata raha.
Kiitikio
Saa ya sala, iliyo heri, Waliochoka sana, watapata raha.
2
Saa heri ya sala, ajapo Mwokozi, Ili awasikie watoto wake, Hutwambia tuweke, miguuni pake, Mizigo yetu yote, tutapata raha.
3
Saa heri ya sala, wawezapo kuja, Kwa Bwana Yesu wanaojaribiwa, Moyo wake mpole, atawarehemu, Waliochoka sana, watapata raha. 4. Saa heri ya sala, tutakapopewa Mibaraka ya roho tukimwamini, Kwa kuamini kweli, hatutaogopa, Waliochoka sana, watapata raha.