140

Nitwae Hivi Nilivyo

1

Nitwae hivi nilivyo, umemwaga damu yako, Nawe ulivyoniita, Bwana Yesu sasa, naja.

2

Hivi nilivyo si langu, kujiosha roho yangu, Nisamehe dhambi zangu, Bwana Yesu sasa, naja.

3

Hivi nilivyo sioni, kamwe furaha moyoni, Daima ni mashakani, Bwana Yesu sasa, naja.

4

Hivi nilivyo kipofu, maskini na mpungufu, Wewe ndiwe u tajiri, Bwana Yesu sasa, naja.

5

Hivi nilivyo mimi tu, siwezi kujiokoa, Na wewe hutanikataa, Bwana Yesu sasa, naja.

6

Hivi nilivyo, mapenzi yamenipa njia wazi, Hali na mali sisazi, Bwana Yesu sasa, naja.