1
Ulimwengu siutaki, namtaka Bwana Yesu, Dunia hunidanganya, Yesu yu mwaminifu.
Kiitikio
Rehema ni ya ajabu, pendo bila kipimo, Wokovu mkamilifu, amana ya uzima.
2
Ulimwengu siutaki, namtaka Bwana Yesu, Kati ya dhoruba kali, yeye wimbo mtamu.
3
Ulimwengu siutaki, namtaka Bwana Yesu, Safarini duniani, yeye furaha yangu.
4
Ulimwengu siutaki, namtaka Bwana Yesu, Msalaba naamini, hata namwona Yesu.