146

Twae Wangu Uzima

1

Twae wangu uzima, sadaka ya daima, Twae saa na usiku, zikutukuze huku.

2

Twae mikono nayo, ifanye upendayo, Twae yangu miguu, kwa uongozi wako tu.

3

Twae sauti yangu, niimbe kwa Mungu tu, Itwae na midomo, ijae neno lako.

4

Twae dhahabu pia, na yote ya dunia, Twae yangu hekima, upendavyo tumia.

5

Nia itwae Mungu, haitakuwa yangu, Twae moyo ni wako, uwe makazi yako.

6

Twae mapenzi yangu, sifa za moyo wangu, Twae kabisa nafsi, niwe wako halisi