1
Yanipasa kuwa naye, Mwokozi Bwana wangu, Akiwa karibu nami, napata nguvu kweli.
Kiitikio
Moyo hauogopi, wala kutikisika. Nitakwenda apendapo, kwa kuwa anilinda.
2
Yanipasa kuwa naye, kwani nategemea, Anaweza kufariji, na maneno matamu.
3
Yanipasa kuwa naye maisha yangu yote, Yakiwapo majaribu, na mashaka yo yote.
4
Yanipasa kuwa naye, katika njia zangu, Macho yake yaongoza, hatua zangu zote.