158

U mwendo Gani Nyumbani?

1

U mwendo gani nyumbani? Mlinzi akanijibu, “Usiku sasa waisha, macheo karibu,” Usihuzunike tena, bali ulemee mwendo, Hata ushike ufalme, kule mwangani juu.

2

Na tena niliuliza, nchi yote ikajibu, “Sasa mwendo watimika, milele karibu,” Usihuzunike tena, ishara kuu zasonga, Na viumbe vyangojea, sauti ya Bwana.

3

Nikamwuliza shujaa, ndivyo kanitia moyo, “Shikilia mapigano, kitambo yaisha,” Usihuzunike tena, kazi ifanywe kwa moyo; Tumeahidiwa tunu tuishapo shinda.

4

Siyo mbali na nyumbani, fikara tamu njiani, yatupoza roho nayo, yafuta machozi, Usihuzunike tena, kitambo tutakutana, Wenye furaha kamili, nyumbani mwa Baba.