1
Unakaribia wakati wa kuja kwa Yesu, Atawachukua watu wake nyumbani juu.
Kiitikio
Tunaiona mishale ya nuru inayopenya giza, Tunaiona mishale ya nuru ya ufufuo.
2
Injili inatangazwa pote kwa mataifa, Bwana wa Arusi atakuja na tarumbeta.
3
Pamoja na malaika zake Bwana arudi, Awapeleke waaminifu wasife tena.
4
Wapenzi waliotengwa kale watakutana, Machozi yao wenye huzuni yatafutika.