1
Hapo Yesu atakapoita, mataifa mbele yake, Tutashindaje kwenye hukumu, mbele ya kiti cha enzi.
Kiitikio
Atakusanya ngano ghalani, atatupa mbali makapi, Tutashindaje hukumuni, siku kuu ya kiyama?
2
Je tutasikia neno tamu, “Vema wewe mtumwa mwema,” Ama wenye uchungu na hofu, tutakatazwa ufalme?
3
Atakubali tu kwa furaha, watoto wake wapendwa, Atawapa mavazi meupe, wakae kitini pake.
4
Hivyo tukeshe nasi tungoje, wenye taa zinazowaka, Tutakapoitwa arusini, tuwe tayari kumlaki.
5
Roho ikielekea mbingu, twangoja wenye saburi, Hata safari yetu iishe, tukae kwake milele.