170

Siitafuti Mali

1

Siitafuti mali, wala utajiri, Nataka kwa yakini, nipate Mwokozi. Chuoni mwa ufalme, niambie Yesu, Jina langu yakini, je limeandikwa?

Kiitikio

Je limeandikwa? Jina langu huko? Kitabuni mbinguni, je, limeandikwa?

2

Dhambi zangu ni nyingi, ni kama mchanga, Lakini damu yako, mwokozi yatosha, Kwani umeahidi, zijapo nyekundu, Zitakuwa nyeupe, ilivyo theluji.

3

Mji mzuri sana, wa majumba makuu, Walipo malaika, mji bila ovu, Wakaapo walio, na mavazi safi, Je limeandikwa, jina langu huko.