176

Ati twonane Mtoni?

1

Ati twonane mtoni? Maji mazuri ya mbingu, Yanatokea mwangani, penye kiti cha Mungu.

Kiitikio

Naam twonane mtoni, watakatifu kwenu ni mtoni, Tutakutanika kule mtoni, penye kiti cha Mungu.

2

Tukitembea mtoni, na Yesu mchunga wetu, Daima tu ibadani, usoni pake kwetu.

3

Tukisafiri mtoni, tutue ulemeao, Wema wa Mungu yakini, una taji na vazi

4

Kwang’ara sana mtoni, cha Mwokozi ni kioo, Milele hatuachani, tumsifu kwa nyimbo.

5

Karibu sana mtoni, karibu tutawasili, Mara huwa furahani, na amani ya kweli.