178

Ukingoni Mwa Yordani

1

Ukingoni mwa Yordani, ninaangalia, Bara nzuri ya Kanaani, ninayotamani.

Kiitikio

Tutakaa pamoja na Yesu, Katika pwani yenye raha, Tutaimba wimbo wa Musa na Kondoo, Milele hata milele.

2

Bara ile ina nuru, nuru ya milele, Kristo jua hutawala, hufukuza giza.

3

Nitapafikia lini, na kubarikiwa, Penye ufalme wa Baba, na kumwona uso.

4

Furaha yangu rohoni ni kuchukuliwa, Siyaogopi mawimbi katika Yordani.