179

Wavunaji Watafurahi

1

Wavunaji watafurahi, pale watakaporudi, Wakiyaleta mavuno, hata Yerusalemu.

Kiitikio

Furaha wataipata, furaha hata milele, Furaha wataipata, wakati wa mavuno.

2

Na siku ile tutaimba, kumshukuru na kumsifu, Bwana Yesu jumbe wetu, kule Yerusalemu.

3

Wavunaji watafurahi, makaoni mwa milele, Yaliyowekwa tayari, kule Yerusalemu.