1
Pana mahali pazuri mno, twapaona kwa mbali sana, Baba yetu angoja pale, amepanga makao yetu.
Kiitikio
Kitambo tu bado, tutakutana ng’ambo pale, Kitambo tu bado, tutakutana ng’ambo pale.
2
Tutaimba pale kwa moyo, nyimbo tamu za wenye heri, Na rohoni hatutaona, tena haja ya kupumzika.
3
Kwa Baba yetu mkarimu, tutatoa shukrani sana, Kwa kipaji cha pendo lake, na baraka anazotupa.