188

Wimbi la Damu

1

Wimbi la damu ya Yesu, linatutakasa, Aliumia kusudi, tupate uzima.

Kiitikio

Wimbi la damu naona, naingia natakaswa, Bwana asifiwe sana, hutakasa hutakasa.

2

Damu inasema kwangu, nasikia mvuto, Inasema moyo wangu, hutakaswa nayo.

3

Naondoka kutembea, kwa nuru ya mbingu, Mavazi yamesafishwa, moyoni ni Yesu.

4

Neema ni ya ajabu, kutakaswa ndani, Na kuwa naye Yesu tu, aliye Mwokozi.