1
Raha yangu yote Bwana, i mbavuni pako, Mimi sina haja tena, ila kifo chako.
2
Mwokozi uliyekufa, nawe ndiwe Mungu, Kifo chako ni kwa dhambi, ziondoe zangu.
3
Nioshe na niwe wako, nawe uwe wangu, Nioshe damuni mwako, liwe fungu langu.
4
Nioshe si miguu tu, osha tangu nyayo, Hata kichwa changu juu, na ndani ya moyo,
5
Na iwe kafara damu, nifanyapo kazi, Hata imani itimu, nikuone Mwokozi.