1
Sauti ya Mchungaji, ninasikia jangwani, Kondoo waliopotea, anawaita warudi.
Kiitikio
Leteni, leteni, leteni toka dhambini, Leteni, leteni, waleteni kwa Yesu.
2
Nani atakayekwenda, amsaidie Mchungaji, Awarudishe zizini, wasife bure gizani.
3
Usikose kusikia, sauti ya Mchungaji, Kondoo waliopotea nenda na kuwatafuta.