194

Twaomba Bwana

1

Twaomba Bwana, umpokee kama mhudumu, Ambaye anajitoa, kuwa mtumishi.

2

Twaomba Bwana, umpokee kama mhudumu, Neno lako alitoe, mwangaza kung’aa.

3

Mwokozi wetu, twaomba na umwandikie, Kitabuni mwako, juu mjumbe wa injili.

4

Silaha zake, apewe kumshinda adui, Vitani awe hodari, mpaka mauti.

5

Yeye ashindaye, Bwana kwa rehema yako, Ile taji ya dhahabu, nawe utampa. Kuweka Kanisa Wakfu