195

Msingi wa Kanisa

1

Msingi wa Kanisa ndiye Yesu Bwana, Kiumbe chake kipya akipenda sana, Kutaka ‘kitafuta alishuka chini, Naye kwa haja yake, akafa mtini.

2

Lina kila kabila kisha ndiyo moja, Wokovu wake una Mwokozi mmoja, Uzazi ni umoja moja tumaini, Chakula ni kimoja, moja tumaini.

3

Watu hustaajabu kwa mashaka yote, Yaipatayo nje hata ndani mwote, Ila watakatifu humwomba wakikesha, Usiku ni kilio, asubuhi raha.

4

Mashaka na taabu hata vita vyake, Vyangoja matimizo ya amani yake, Ndipo kwa macho yetu twone utukufu, Kanisa ya kushinda, itastarehe juu