1
Mungu wetu yeye mwamba, kimbilio taabuni, Msaada penye shida, ulio karibu sana.
Kiitikio
Mwamba wetu kutupumzisha, yu kivuli kuburudisha, Huongoza katika njia, kimbilio taabuni.
2
Mchana usiku yeye, kimbilio taabuni, Hivyo hatutaogopa, kwani yu karibu sana.
3
Iwayo yote Yeye tu, kimbilio taabuni, Twamjua Yeye mlinzi, aliye karibu sana.
4
Mungu wetu ficho kwetu, kimbilio taabuni, Siku zote uwe boma, lililo karibu sana.