23

Yesu Furaha ya Moyo

1

Yesu furaha ya moyo, hazina ya pendo na nuru. Yote yatupendezayo, yasilinganishwe nawe.

2

Kweli yako ya daima, wawajibu wakwitao, Ni siku zote u mwema, kwao wakutafutao.

3

U Mkate wa Uzima, kupokea ni baraka, Twanywa kwako u kisima, roho zikiburudika,

4

Mwokozi twakutamani, kwako roho hutulia, Twakushika kwa imani, nawe watubarikia.

5

Yesu, ndiwe kwetu mwanga, tufurahishe daima, Giza la dhambi fukuza, uwe mwanga wa Uzima.