24

Jina Lake Yesu Tamu Tukilisikia

1

Jina lake Yesu tamu, tukilisikia, Hutupoza tena hamu, hutuondolea.

2

Roho iliyoumia, kwalo hutibika, Chakula njaani pia, raha tukichoka.

3

Jina hili ni msingi, ngao, ngome, mwamba, Kwa hili napata vingi, kwangu ni akiba.

4

Yesu, Mchunga, Rafiki, Mwalimu, Kuhani, Mwanzo, Mwisho, na Amina, mali yangu yote!

5

Moyo wangu hauwezi, kukusifu kweli, Ila sifa zangu hizi, Bwana zikubali.