27

Tena Mwokozi Twalitukuza

1

Tena Mwokozi twalitukuza, Jina lako lenye kupendeza, Twangojea neno la amani, Kabla hatujakwenda nyumbani.

2

Tupe amani njiani mwetu, Wewe u mwanzo u mwisho wetu, Dhambini kamwe isiingie, Midomo ikutajayo wewe.

3

Utupe amani usiku huu, Ili gizani kuwe nuru kuu, Tulinde kwa kuwa kwako Bwana, Usiku ni sawa na mchana.

4

Tupe amani ulimwenguni, Ndiyo dawa yetu majonzini, Na ikitwita sauti yako, Tupe amani milele kwako.