1
Jina lake Yesu tamu, lihifadhi moyoni, Litakufariji ndugu, enda nalo po pote.
Kiitikio
Jina la thamani, (Jina la ) (thamani) Tumai la dunia, Jina la thamani, (Jina la thamani–tamu) Furaha ya mbinguni.
2
Jina la Yesu lafaa, kama ngao vitani, Majarabu yakisonga, omba kwa jina hili.
3
Jina hili la thamani, linatufurahisha, Anapotukaribisha, na tunapomwimbia.
4
Mwisho wa safari yetu, tutakapomsujudu, Jina hili tutasifu, furaha ya mbinguni.