1
Yesu nakupenda u mali yangu, Anasa za dhambi sitaki kwangu, Na Mwokozi aliyeniokoa, Sasa nakupenda kuzidi pia.
2
Moyo umejaa mapenzi tele, Kwa vile ulivyonipenda mbele, Uhai wako ukanitolea Sasa nakupenda kuzidi pia.
3
Ulipoangikwa msalabani, Tusamehewe tulio dhambini, Taji ya miiba uliyoivaa, Sasa nakupenda kuzidi pia.
4
Mawanda mazuri na masikani, Niyatazamapo huko mbinguni, ‘Tasema na taji nitakayovaa, Sasa nakupenda kuzidi pia.