1
Pendo lako Ee Mwokozi, hushinda pendo zote, Kaa nasi ndani yetu, furaha ya mbinguni, Yesu u rehema tupu, safi na kusamehe, Mfariji mwenye huzuni, yaondoe machozi.
2
Roho yako ya upendo, tuma kwa kundi lako, Hebu tuirithi raha, iliyoahidiwa, Uondoe moyo mbaya, u mwanzo, tena mwisho, Timiza imani yetu, ili tuwekwe huru.
3
Yesu uje kwetu sasa, tupokee huruma, Rudi kwetu tena kamwe, usituache pekee, Tungekutukuza leo, pamoja na malaika, Imba na kutoa sifa, ingia kwa ibada.
4
Sasa Bwana kazi yako, imalize moyoni, Takasa hekalu lako, wokovu kamilisha, Safisha viumbe vyako, katika wakati huu, Tupumzike toka dhambi, tuingie mbinguni.