1
Jina la Yesu, salamu! lisujudieni, Ninyi mbinguni, hukumu na enzi mpeni. Ninyi mbinguni, hukumu na enzi mpeni.
2
Enzi na apewe kwenu, watetea dini; Mkuzeni Bwana wenu, na enzi mpeni. Mkuzeni Bwana wenu, na enzi mpeni.
3
Enyi mbegu ya rehema, nanyi msifuni Mmeponywa kwa neema, na enzi mpeni. Mmeponywa kwa neema, na enzi mpeni.
4
Wenye dhambi kumbukeni, ya msalabani. Kwa furaha msifuni, na enzi mpeni. Kwa furaha msifuni, na enzi mpeni.
5
Kila mtu duniani msujudieni, Kote-kote msifuni, na enzi mpeni. Kote-kote msifuni, na enzi mpeni.
6
Sisi na wao pamoja tu mumo sifani. Milele sifa ni moja, ni enzi mpeni. Milele sifa ni moja, ni enzi mpeni.