1
Na tumwabudu huyo Mfalme, Sifa za nguvu zake zivume; Ni ngao, ni ngome, Yeye milele, Ndizo sifa zake kale na kale.
2
Tazameni ulimwengu huu, Ulivyoumbwa, ajabu kuu; Sasa umewekwa pahali pake, Hata utimize majira yake.
3
Kwa ulinzi wako, kwetu Bwana, Twakushukuru, U mwema sana; Hupewa chakula kila kiumbe, Kila kitu kina mahali pake.
4
Wanadamu tu wanyonge sana, Twakutumaini Wewe, Bwana; Kamwe haupungui wako wema, Mkombozi wetu, Rafiki mwema.