1
Nipe Biblia nyota ya furaha,wapate nuru wasafirio, Hakuna la kuzuia amani, kwani Yesu alituokoa.
Kiitikio
Nipe Biblia neno takatifu, nuru yake itaniongoza, Sheria na ahadi na upendo, hata mwisho vitaendelea.
2
Nipe Biblia nihuzunikapo, ikinijaza moyoni dhambi, Nipe neno zuri la Bwana Yesu, nimwone Yesu Mwokozi wangu.
3
Nipe biblia nipate kuona, hatari zilizo duniani, Nuru ya neno lake Bwana Yesu, itaangaza njia ya kweli.
4
Nipe Biblia taa ya maisha, mfariji tunapofiliwa, Unionyeshe taa ya mbinguni, nione utukufu wa Bwana.