1
Napenda kuhubiri, habari ya Yesu, Ya Bwana wa fahari, na pendo lake kuu. Kuhubiri napenda, kwa hali na mali, Mwenyewe nimeonja, najua ni kweli.
Kiitikio
Napenda kuhubiri, kisa cha Bwana Yesu, Cha Bwana wa fahari, na pendo lake kuu.
2
Napenda kuhubiri, mambo ya ajabu, Na tukiyafikiri, yapita dhahabu, Kuhubiri napenda, ya yaliyonifaa, Nami sana napenda, hayo kukwambia.
3
Napenda kuhubiri, hunifurahisha, Tamu yake habari, haiwezi kwisha, Napenda kuhubiri, wa gizani nao, Hawana mhubiri, wa kueleza chuo.
4
Kuhubiri napenda, hata wajuao, Kusikia hupenda, kama wenzi wao, Nako kwenye fahari, nikiimba wimbo, Nitaimba habari, ya Mwokozi huyo.