59

Fanyeni Kazi Zenu

1

Fanyeni kazi zenu, usiku si mbali, Kesheni saa zenu, vumilieni, Kwa Yesu tumikeni, na hiyo Injili, Sana wahubirini, watu wa mbali.

2

Fanyeni kazi zenu, giza lasogea, Na wengi wenzi wenu, wamo gizani, Msipoteze moja, dakika ni hizi, Bwana atarejea, mwisho wa kazi.

3

Fanyeni kazi zenu, hivi jua lachwa: Wote walio kwenu apenda Mungu Na sisi tumjuaye na tuwafundishe Ili Yesu ajaye tumfurahishe.