60

Pengine Siyo Mlimani

1

Pengine siyo mlimani, utakaponiita, Pengine siyo baharini, wala palipo vita, Lakini unaponiita, na njia siijui, Bwana nitajibu ni tayari, kwenda uniagizapo.

Kiitikio

Ukiwa pamoja nami Bwana, mlimani baharini, Niende utakaponiita; na fuata uendako.

2

Pengine leo kuna neno, neno tamu la pendo, Ambalo Yesu anataka, ninene kwa upole, Ukiwa pamoja nami Bwana, nitamtafuta leo, Yule aliyepotea mbali, nitasema upendavyo.

3

Pahali pako bila shaka, pa kuvuna shambani, Kazi niwezayo kufanya, kwa Yesu Mkombozi, Hivi nikikutegemea, kwa kuwa wanipenda, Mapenzi yako nitayafanya, na niwe upendavyo.